NA ALBERT G.SENGO/MWANZA
WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega ametembelea na kukaguwa eneo la mradi wa upanuzi wa Daraja la Mabatini na barabara unganishi yenye urefu wa meta 590, wilayani Nyamagana, jijini Mwanza na kukuta mradi huo ukiwa umekamilika kwa asilimia 93 hivyo kuanza kupitika. Waziri Ulega pia amempongeza mkandarasi kwa kazi anayofanya. “Wananchi wameridhika. Msongamano wa magari nao umepungua kwa kiwango kikubwa,” alisema Ulega na kuongeza kuwa upanuzi wa barabara mbili kwenda na kurudi umeongeza ufanisi wa usafiri katika eneo hilo. Zaidi fuatilia video hii........ #jembefmtz #samiasuluhuhassan #mwanza #waziriWaUjenzi #WaziriUlegaFriday, December 12, 2025
WAZIRI ULEGA "SITOONGEZA HATA SEKUNDE UJENZI BARABARA NA DARAJA LA MKUYUNI" - MKANDARASI ATOBOA SIRI
NA ALBERT G.SENGO/MWANZA
Mnamo Disemba 5, mwaka huu 2025 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt, Mwigulu Nchemba alifanya ziara jijiji Mwanza kuzitembelea familia zilizopata madhara ya vurugu za uchaguzi Mkuu wa Oct 29/2025. Pamoja na kuzungumza na wakazi wa jiji hili la miamba, pia Waziri Mkuu alipokea kero sugu ya kutokamilika kwa barabara na madaraja kadhaa likiwemo lile la eneo muhimu la Mkuyuni. Katika sehemu ya majibu yake Mhe. Waziri mkuu alitoa agizo kwa Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdalah Ulega kuja na kulikagua daraja hilo haraka iwezekanavyo na kutoka na suluhisho. Mwanahabari wetu Albert G. Sengo anakuja hapa na taarifa kamili. Lakini kwanza hebu tujikumbushe kauli ya Waziri Mkuu aliyoitoa mnamo Disemba 5 2025.Wednesday, December 10, 2025
USALAMA UMEENDELEA KUIMARIKA NCHINI- POLISI
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime amesema hali ya usalama ni shwari kote nchini Tanzania na shughuli za kiuchumi na kijamii zinaendelea kama kawaida nchi nzima baada ya mapumziko ya sherehe za sikukuu ya Uhuru wa Tanzania bara jana Jumanne Disemba 09, 2025.
Kulingana na taarifa yake kwa Vyombo vya habari, Jeshi la Polisi kwa ushirikiano na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vitaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha amani na usalama unaendelea kuimarika nchini ili hata wale wachache wenye hofu waweze kutoka na kuendelea na shughuli zao za kila siku za kujitafutia riziki na kupata huduma za kijamii wanazo hitaji.
"Aidha tunawashukuru na kuwapongeza wananchi wote kwa nafasi zao kwa namna wanavyoendelea kuwakataa na kuwapuuza wale wanaohamasisha na kuchochea vurugu na ukiukwaji wa Sheria za nchi kupitia mitandao ya kijamii na njia zingine." Amesema Misime.
CHELSEA YAKUNG'UTWA, BARCELONA YAPINDUA MEZA, LIVERPOOL YANG'ARA ULAYA.
Usiku wa jana umeshuhudia matokeo tofauti katika michezo ya Ulaya, huku Chelsea ikipoteza ugenini, Liverpool ikiwahi dakika za mwisho, na Barcelona ikitoa burudani ya kupindua meza.
Atalanta 2-1 Chelsea
Chelsea imekubali kipigo cha 2-1 dhidi ya Atalanta kwenye mchezo uliochezwa ugenini.
Matokeo:
55’ Gianluca Scamacca (Atalanta)
83’ Charles De Ketelaere (Atalanta)
26’ Pedro (Chelsea)
The Blues walitangulia kupata bao mapema kupitia Pedro, lakini Atalanta walionyesha uimara kipindi cha pili na kufanikiwa kusawazisha kisha kuongeza bao la ushindi dakika za lala salama.
Inter Milan
0-1
Liverpool
Liverpool imeondoka San Siro na ushindi mwembamba wa 1-0, bao pekee likifungwa dakika ya 88 na Dominik Szoboszlai.
88’ Szoboszlai
The Reds walionyesha uthabiti mkubwa na subira iliyowalipa mwishoni mwa mchezo.
Barcelona
2-1
Eintracht Frankfurt
Barcelona imepindua matokeo kutoka 1-0 na kushinda 2-1 dhidi ya Eintracht Frankfurt.
50’ Kounde
53’ Kounde
21’ Knauff (Frankfurt)
Bao mbili mfululizo za Jules Kounde ndani ya dakika tatu ziliipa Barca ushindi muhimu baada ya hiviwana kuanza nyuma.
GAMONDI ATEMA MAJINA MAKUBWA STARS KUELEKEA AFCON 2025.


Tuesday, December 9, 2025
MECHI ZA LEO UEFA NI PRESHA TUPU....
Italia kutakuwa na mechi ya kukata Inter Milan vs Liverpool ambao hivi karibuni wamekuwa na matokeo ambayo hayaridhishi kabisa kwani kwenye mechi 13 amabzo amecheza ameshinda 3 pekee. Mara nyingi hawa wawili kukutana ilikuwa kwenye fainali na Jogoo wa Anfield alipoteza.
Vijana wa Diego Simeone, Atletico Madrid watakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya PSV kutoka kule Uholanzi lakini pia imeweza kupata matokeo dhidi ya timu kubwa kwenye michuano hii.
AS Monaco atakuwa nyumbani kupepetana dhidi ya Galatasaray ambao walipoteza mechi yao iliyopita wakiwa nyumbani. Mwenyeji yeye alitoa sare, hivyo pointi 3 ni muhimu kwa timu zote siku ya leo.
Marseille yeye atakuwa kibaruani kumenyana vikali dhidi ya Union St.Gilloise ambao wanahitaji ushindi siku ya leo ili wasogee mbele kwenye michuano hii. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni hakuna kwani wote wana pointi sawa.
Bayern Munich yeye atakipiga dhidi ya Sporting CP ambapo mpaka sasa kwenye mechi 8 ambazo amecheza amekusanya pointi 10 huku vijana wa Kompany wao wakichukua pointi 12. Mwenyeji ametoka kupoteza huku mgeni yeye akishinda.
Kwa upande wa Chelsea wao watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Atalanta baada ya mechi iliyopita kushinda, halikadhalika kwa wenyeji nao walishinda.
Vijana wa Hans Flick, FC Barcelona watakuwa nyumbani kusaka ushindi dhidi ya Eintracht Frankfurt ambao wana pointi 4 pekee hadi sasa huku Wacatalunya wao wakiwa na pointi 7. Barca wanahitaji ushindi kwa namna yoyote ile ili wajiweke kwenye nafasi nzuri ya michuano hii.
Tottenham Spurs atakuwa kibaruani kukipiga dhidi ya Slavia Prague ambao kwenye mechi 5 wameambulia pointi 3 pekee. Huku wenyeji wao wakiwa na pointi 8 hadi sasa.
"MSIWE NA HOFU MWANZA HALI NI SHWARI CLIP INAYOSAMBAA NI YA TAREHE 31 OCTOBA 2025" RC MTANDA
NA ALBERT G. SENGO/MWANZA
🛑Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, ametoa taarifa rasmi kuhusu hali ya usalama mkoani Mwanza, huku akikanusha vikali uvumi unaoenezwa mitandaoni kuhusu kuwepo kwa maandamano katika jiji hilo. Katika taarifa hiyo, Mhe. Mtanda ameeleza kwa uwazi kuwa video inayosambazwa mtandaoni si ya leo, bali ni tukio la zamani linalotumiwa kupotosha umma. 👉 Fuatilia video kamili kupitia #youtube chanel yetu hapa ujue alichokisema kwa kina Mkuu wa Mkoa juu ya usalama, uzushi wa maandamano, na msimamo wa serikali mkoani humo.Hakuna huduma, hakuna pilikapilika kama ilivyozoeleka, vituo vingi vya wauzaji wa mafuta na gesi jijini Mwanza, vimesitisha huduma kwa siku ya leo.
Ni tofauti na ilivyozoeleka, leo magari ni ya kuhesabu katika barabara hii yenye pilika pilika hapa jijini Mwanza.
Muonekano wa barabara ya kuelekea Kirumba.
Muonekano wa barabara ya Makongoro uelekeo wa uwanja wa ndege jijini Mwanza.
Muonekano kutoka barabara ya Nyerere hii ni barabara ya kuelekea mitaa iliyozoeleka kwa pilikapilika nyingi ya Rufiji na Uhuru, lakini leo watu wachache na magari ya kuhesabu.
Hakuna huduma kwa siku ya leo.
Muonekano.
Monday, December 8, 2025
VITALIS MAYANGA AFUNGIWA MECHI TANO NA KUTOZWA FAINI.

Mshambuliaji wa Mbeya City, Vitalis Mayanga amefungiwa kucheza mechi tano sambamba na kutozwa faini ya Tsh Milioni 1 kwa kosa la kumpiga kiwiko kwa makusudi beki wa kushoto wa Simba SC, Anthony Mligo.
Uamuzi huo umetolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) katika taarifa ya TPLB leo Desemba 8, 2025.
SIMBACHAWENE: HAKUNA TISHIO LA KUZIMWA INTERNET TANZANIA, HALI YA USALAMA NI SHWARI.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, amesema kuwa hatua ya kuzima mtandao wa intaneti nchini ni chaguo la mwisho kabisa, na kwa sasa hakuna sababu yoyote inayoashiria uwezekano wa TCRA kuchukua hatua hiyo kuelekea maadhimisho ya Uhuru kesho, Desemba 09, 2025.
Akizungumza leo, Desemba 08, 2025, Simbachawene amesema kuwa taarifa zinazosambaa mtandaoni kuhusu hofu ya kuzimwa kwa internet hazina msingi, kwani hali ya kiusalama nchini imo katika kiwango cha kuridhisha.
“Kuhusu kuzimwa mtandao, kwa sababu nyenzo kubwa inayotumika na hawa wanaharakati wa mitandaoni ni taarifa za taharuki… mpaka sasa hatujaona tishio lolote la kusema mtandao umekuwa tatizo,” amesema.
Ameeleza kuwa mitandao ya intaneti ina mchango mkubwa katika maisha ya kila siku ya Watanzania, kuanzia shughuli za kibenki, usafiri, mawasiliano hadi huduma mbalimbali za kijamii, hivyo serikali haina sababu ya kuuzuia bila msingi wa kiusalama ulio wazi.
“Tufahamu mtandao huu ndio unatumika kutoa huduma nyingi za kijamii. Kwa hiyo kuzima internet ni chaguo la mwisho sana pale ambapo hali ikiwa mbaya… lakini mpaka sasa, tunaoangalia usalama wa nchi, tunaona hali ni shwari,” amesema.
Simbachawene amesisitiza kuwa hadi sasa hakuna tishio lolote linaloweza kuilazimu TCRA kuzima huduma za intaneti, na Watanzania wanapaswa kuendelea na shughuli zao kama kawaida bila wasiwasi.
WANAFAMILIA 9 WALIOKUFA KATIKA AJALI WAKIENDA MAZISHI YA JAMAA YAO WAZIKWA PAMOJA

Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa ndugu na marafiki waliofariki kwa ajali hiyo.
Safu za majeneza meupe zilikaa kimya chini ya hema, picha ya kuhuzunisha ilinaswa na kusambazwa mtandaoni na mwandishi wa habari Bruce Kanzika.
Waombolezaji kutoka kila aina ya maisha walikusanyika kuwaaga waathiriwa ambao maisha yao yalikatizwa katika wakati mmoja, wa kuhuzunisha.
Msiba huo umetikisa kijiji cha Sango ambapo familia ilikuwa ikisubiri kwa hamu kuwasili kwa jamaa zao kwa mazishi ya bibi yao, Mama Perpetua Tsivona.
Huenda swali likawa:- Jeh Waathiriwa walikuwa wakisafiri kwenda wapi?
Gari hilo, lililokuwa limebeba abiria 15, lilikuwa njiani kutoka Nairobi kwenda Lugari wakati ajali hiyo ilipotokea, na kuhitimisha safari iliyokusudiwa kuunganisha familia yenye huzuni.
Simu iliyovunja mioyo ya familia nzima Kwa wazazi wa marehemu, maumivu bado hayajafikirika. Irene Haron, mama wa watoto tisa, alikumbuka kupokea simu kutoka kwa watoto wake, akimhakikishia kwamba walikuwa karibu na Naivasha na wangekuwa nyumbani alasiri.
Muda mfupi baadaye, ulimwengu wake ulivunjika. “Sijui hata niseme nini. Watoto wangu wote tisa, wote wameenda,” alisema, akitetemeka huku akijitahidi kuelezea huzuni yake. “Kila ninapofikiria kuhusu hilo, mimi hutetemeka tu.” Mumewe, Mzee Haron Tsivona, anakumbuka kupokea simu kutoka kwa nambari ambayo hajui wakati yeye na jamaa wengine walikuwa wakiimba nyumbani kwa mama yake.
Alipopokea simu, alikuwa polisi wa trafiki akimjulisha kwamba wanafamilia wake walikuwa wamehusika katika ajali. “Dakika chache tu mapema, watoto wangu walikuwa wamepiga simu kusema walikuwa karibu kurudi nyumbani,” alisimulia, sauti yake ikiwa nzito kwa kutoamini.
Bajeti ya mazishi:-
Wakati wanandoa hao wakikabiliwa na kazi isiyofikirika ya kuwazika watoto wao wote tisa, mzigo wa kifedha umeongeza safu nyingine ya uchungu. Familia ilikuwa na bajeti ya KSh milioni 4.5 kufidia gharama za mazishi, kiasi ambacho ni zaidi ya uwezo wao, na kulazimisha kutafuta msaada kutoka kwa wasamaria wema.
Jamaa aliyetambuliwa kama Paulo Wawire alishiriki matumaini na ndoto ambazo watoto hao wa marehemu walikuwa nazo kwa wazazi wao, akiongeza kuwa walikuwa wameanza tu kupanga kujenga nyumba mpya kwa ajili ya wazazi wao. Miongoni mwa waliotembelea familia hiyo alikuwa Mbunge wa Lugari Nabii Nabwera ambaye alitoa mchango wa KSh milioni 1 kutoka kwa Rais William Ruto ili kusaidia mipango ya mazishi.
Je, ajali hiyo ilikuwa na manusura?
Huku Chevaywa akijiandaa kuwazika tisa wake, manusura wa ajali hiyo mbaya wanaendelea kulazwa hospitalini wakipokea matibabu. Kijiji hicho, kikiwa kimezidiwa na huzuni, kinashikilia umoja na maombi huku kikikabiliana na moja ya nyakati za giza zaidi katika historia yake. Kwa familia ya Haron, njia ya kuelekea uponyaji itakuwa ndefu, lakini jamii imeapa kuitembea nao, hatua moja, siku moja baada ya nyingine.
IMBEJU NI ZAIDI YA MPANGO WA KUTOA MIKOPO CRDB BANK
Friday, December 5, 2025
MANISPAA YA KIBAHA YAJA NA MPANGO WA KUSAIDIA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI
NA VICTOR MASANGU, KIBAHA
CCM PWANI HAWANA DOGO WAMPA MAUWA YAKE RAIS DKT.SAMIA KWA HOTUBA YAKE YENYE TIJA KWA TAIFA
Na Victor Masangu,Kibaha
Tuesday, December 2, 2025
DC KIBAHA AKABIDHI GARI LITAKALOTUMIKA KUBORESHA HUDUMA KATIKA DIVISHENI YA ARDHI
DR. NICAS KUNOGILE AKWEA PIPA NAFASI YA UMEYA HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA
Na Victor Masangu,Kibaha
Monday, December 1, 2025
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI ATOA MAAGIZO KWA WAKURUGENZI JUU YA KAMPENI YA KUWAPELEKA WATOTO SHULE
MWANDISHI:- VICTOR MASANGU, PWANI MTANGAZAJI:- ALBERT G.SENGO Naibu waziri Ofisi ya Waziri mkuu Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Reuben Kwagilwa anayeshugulikia masuala ya elimu amewaagiza wakurugenzi wote nchi nzima kufanya kampeni kwa ajili ya kuwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka na kuwaandikisha watoto wao shule za awali na msingi pindi ifikapo Januari mwaka 2026, Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja ambapo ameweza kugagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambayo imejengwa katika eneo la Disunyara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani na kumwagiza mkandarasi kumaliza mradi huo kwa muda uliopangwa.






.png)
.png)
.png)
.png)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.png)
.png)
.png)
.png)
.png)




.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)