Tuesday, December 2, 2025
DC KIBAHA AKABIDHI GARI LITAKALOTUMIKA KUBORESHA HUDUMA KATIKA DIVISHENI YA ARDHI
DR. NICAS KUNOGILE AKWEA PIPA NAFASI YA UMEYA HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA
Na Victor Masangu,Kibaha
Monday, December 1, 2025
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI ATOA MAAGIZO KWA WAKURUGENZI JUU YA KAMPENI YA KUWAPELEKA WATOTO SHULE
MWANDISHI:- VICTOR MASANGU, PWANI MTANGAZAJI:- ALBERT G.SENGO Naibu waziri Ofisi ya Waziri mkuu Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Reuben Kwagilwa anayeshugulikia masuala ya elimu amewaagiza wakurugenzi wote nchi nzima kufanya kampeni kwa ajili ya kuwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka na kuwaandikisha watoto wao shule za awali na msingi pindi ifikapo Januari mwaka 2026, Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja ambapo ameweza kugagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambayo imejengwa katika eneo la Disunyara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani na kumwagiza mkandarasi kumaliza mradi huo kwa muda uliopangwa.
Sunday, November 30, 2025
STANBIC BANK MWANZA YAFANYA KWELI SEKTA YA AFYA MWANZA
NA. ALBERT G.SENGO/MWANZA
Benki ya Stanbic imeonesha tena dhamira yake ya kusaidia jamii kwa vitendo, baada ya kukabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 19 kwa uongozi wa Mkoa wa Mwanza. Vifaa hivyo ambavyo ni pamoja na vitanda vya wagonjwa, mashuka na viti mwendo, vitapelekwa katika Hospitali za Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, ili kusaidia katika utoaji wa huduma bora za afya. Kutoka kwa mwanahabari wetu Albert G. Sengo., anashuka na taarifa kamiliWednesday, November 26, 2025
DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA
Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Novemba 26, 2025) wakati akifungua Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Usafiri Endelevu Ardhini katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa haitakuwa uungwana kuona baadhi ya watu wakilipa adhabu papo hapo wanapokosea ilhali wengine wakiachwa kupita bila kuchukuliwa hatua.
Amewaonya baadhi ya viongozi na madereva wa Serikali ambao wanaelewa sheria vizuri lakini bado wanazikiuka kwa makusudi. “Ni muhimu kuwasaidia watumiaji wa vyombo vya usafiri kama bodaboda na bajaji ambao kwa sehemu kubwa wanaweza kuwa hawazielewi sheria kikamilifu, badala ya kuwaadhibu kwa upendeleo.”
Dkt. Mwigulu amesisitiza umuhimu wa kuwapa Watanzania wote heshima na kuhakikisha sheria zilizowekwa zinatekelezwa kwa maslahi ya wote na kuongeza kuwa endapo zipo sheria ngumu kutekelezeka, basi zibadilishwe ili kila Mtanzania anufaike.

Ameviagiza vyombo vya usimamizi wa sheria vihakikishe kuwa watumiaji wote wa vyombo vya usafiri wanazingatia usimamizi wa sheria na kuchukua hatua kwa yoyote anayevunja sheria akamatwe na kuchukuliwa hatua bila kuonewa aibu.
“Inaudhi mtu amebeba mgonjwa anafuata sheria, halafu mwingine anapita tu anavunja sheria, hapati adhabu. Mlalahoi akivunja sheria anapata adhabu, tunawapa kazi watekeleza sheria kuwaomba radhi watu waliovunja sheria. Naelekeza kila mtu afuate sheria, uwe wa serikalini ama uwe binafsi, tumeweka sheria, zifuatwe kama zilivyo.”
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maadhimisho hayo, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa alisema sekta ya uchukuzi ni mojawapo ya sekta wezeshi za uchumi duniani kota na kwamba watu wanahitaji njia za uchukuzi ili kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na wadau wa usafirishaji nchini ili kuhakikisha masuala ya nishati safi yanapewa kipaumbele. Akitoa mfano, Waziri Mbarawa alisema: “Uendeshaji wa reli ya kisasa (SGR) unatumia nishati ya umeme, mabasi ya mwendokasi njia ya Mbagala yanatumia gesi asili na baadhi ya taxi na bajaji zinatumia gesi asili.”
Tuesday, November 25, 2025
WATAALAM WA KIMATAIFA WATOA MWELEKEO MPYA WA UCHUMI KATIKA KONGAMANO LA TIA MWANZA
TIA Yasistiza Utafiti na Ubunifu Katika Kuchochea Uchumi – Kongamano la Kimataifa la 4 la Usimamizi wa Biashara na Ukuaji wa Uchumi Lafana Mwanza
Mwanza, 25 Novemba 2025 – Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) leo imeongoza Kongamano la 4 la Kimataifa la Usimamizi wa Biashara na Ukuaji wa Uchumi, lililofanyika katika Ukumbi wa Nyerere, Gold Crest Hotel jijini Mwanza, likiwa na ujumbe mahsusi unaoangazia nafasi ya ubunifu, uvumbuzi na biashara katika kuchochea uchumi endelevu.
Akizungumza kumwakilisha mgeni Rasmi, Benjamin Magai ambaye ni Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali , amesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika utafiti wa kisayansi, kama njia ya kutoa suluhisho la changamoto za kijamii na kiuchumi. Akibainisha kuwa utafiti ndio injini ya maendeleo, hasa katika maeneo kama ubunifu, teknolojia, tathmini, miundombinu na mikakati ya maendeleo yenye tija.
Dira ya Maendeleo ya 2050 Yawekwa 
Dhima: Uvumbuzi, Ubunifu na Biashara kwa Uchumi Endelevu
Kongamano la mwaka huu limebeba kaulimbiu “Uvumbuzi, Ubunifu na Biashara kwa Uchumi Endelevu.” Kaulimbiu hiyo imegawanywa katika mada 11, huku machapisho 41 ya tafiti yakitarajiwa kuwasilishwa.
Prof. Pallangyo alisema kuwa kabla ya mawasilisho ya tafiti, kutakuwa na watoa mada wakuu 8 (Keynote Speakers) kutoka ndani na nje ya Tanzania, ambao ni wabobezi katika nyanja zao. Miongoni mwao ni:
Watoa Mada Wakuu ni kama ifuatavyo:-
Katika hotuba yake ya ufunguzi, Afisa Mtendaji Mkuu wa TIA, Prof. William Amos Pallangyo, amekumbusha kuwa TIA ni mojawapo ya taasisi kongwe na muhimu nchini katika kutoa elimu ya uhasibu, ugavi na fani nyingine za biashara. Ikiwa na kampasi 8 nchini na zaidi ya wanafunzi 32,000, na taasisi hiyo imeendelea kuimarisha mfumo wa mafunzo unaozingatia umahiri (Competence Based Training – CBET), sambamba na kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam.
Baada ya mawasilisho ya tafiti, TIA imetangaza kuwa itachapisha kitabu maalum kitakachokusanya mapendekezo ya watafiti juu ya namna bora ya kutatua changamoto katika sekta za biashara na uchumi. Kitabu hicho kitasambazwa kwa wadau muhimu, ikiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama mchango wa TIA katika kusaidia sera na maamuzi ya maendeleo.
Katika kuunga mkono juhudi za Serikali kukuza utalii, washiriki wa kongamano wamepangiwa kutembelea vivutio vya Jiji la Mwanza. Hii ni sehemu ya mkakati wa kutumia kongamano kama nyenzo ya kuhamasisha utalii wa ndani.
Monday, November 24, 2025
UBUNIFU WA KIPEKEE KISIWA CHA SAANANE WAIBUKA A TUZO
![]() |
| Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane, Kamishna Msadizi wa Uhifadhi Dkt. Tutindaga George, akipokea Tuzo ya Ubunifu wa Mazao ya Utalii, jijini Dar es Salaam. |
Ubunifu wake wa kipekee umevuka mipaka ya kawaida na sasa umetambuliwa kitaifa!
![]() |
| Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Dkt. Tutindaga George, akionesha Tuzo yake ya Ubunifu wa Mazao ya Utalii. |
SIMBA SC YACHAPWA 1-0 NA PETRO DE LUANDA LIGI YA MABINGWA DAR

TIMU ya Simba SC imeanza vibaya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuchapwa bao 1-0 na Petro de Luanda ya Angola katika mchezo wake wa kwanza wa Kundi D jioni ya Jumapili ya tarehe 23 Nov 2025 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Bao pekee lililoizamisha Simba SC limefungwa na kiungo Mreno, Bernardo Oliveira Dias dakika ya 78 alipofumua shuti la umbali wa Nita 20 ambalo lilimbabatiza beki raia wa Afrika Kusini, Rushine De Reuck na kubadili njia likimpoteza mwelekeo kipa namba moja Tanzania, Yakoub Suleiman Ali.
Mechi nyingine ya Kundi D jana Espérance ililazimishwa sare ya bila mabao na Stade Malien ya Mali Uwanja wa Hammadi Agrebi, Tunisde Jijini Tunis nchini Tunisia.
Mechi zijazo Simba SC itasafiri kuwafuata Stade Malien Novemba 29 Uwanja wa Machi 26 Jijini Bamako nchini Mali, wakati Petro de Luanda wanarejea nyumbani kuwakaribisha Espérance de Tunis November 29. Uwanja wa Novemba 11 Jijini Luanda.
MUDATHIR APANDA JUKWAANI KUMFUATA RAIS ENG. HERSI BAADA YA GOLI LA DUBE
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee katika mchezo huo wa kwanza wa Kund B, mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Mpumelelo Dube dakika ya 58 akimalizia pasi ndefu ya kiungo mzawa, Mudathir Yahya Abbas.



Saturday, November 22, 2025
CLEMENCE MWANDAMBO ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mtuhumiwa alikamatwa majira ya saa 5:20 asubuhi, kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa polisi kwamba alikuwa ametumia kurasa zake za “Facebook” na “Instagram” kuchapisha taarifa zilizodaiwa kuhamasisha taharuki na kuweza kusababisha uvunjifu wa amani. Polisi wamesema mara baada ya kupokea taarifa hizo, waliendesha uchunguzi wa haraka ambao ulipelekea hatua ya kumkamata kwa ajili ya kuendelea na mahojiano.
Jeshi la Polisi limeeleza kuwa mitandao ya kijamii imeendelea kuwa chanzo kikubwa cha kusambaa kwa taarifa mbalimbali, hivyo wananchi wanatakiwa kutumia majukwaa hayo kwa uangalifu na kufuata sheria za nchi.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa uchunguzi bado unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Aidha, Jeshi la Polisi limewahimiza wananchi kutoa ushirikiano pindi wanapobaini matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, ikiwemo uchochezi, uongo, matusi, au taarifa zinazoweza kuleta mgawanyiko katika jamii.
Kukamatwa kwa mwalimu huyo kumeibua mijadala mitandaoni, baadhi ya wananchi wakisema kuwa vyombo vya habari na mamlaka zinapaswa kufafanua zaidi kuhusu ni aina gani ya maneno yanaweza kufasiriwa kama uchochezi ili kuepusha mkanganyiko.
HAKIMU AKATAA KUTUPA JELA MWANAFUNZI ALIYEFIKISHWA KORTINI KWA KUIBA POMBE.
Mahakama ya Thika imevuta hisia za umma baada ya Hakimu Mkuu Stella Atambo kukataa kumhukumu kijana anayedaiwa kujaribu kuiba pombe ya whisky.
Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 23, alidaiwa kujaribu kuiba pombe yenye thamani ya KSh1,800 kutoka kwa Duka Kuu la Naivas. Uamuzi wa Hakimu Mkuu Atambo ulifuatia mazungumzo mafupi yaliyojaa maswali, ushauri, na msukumo wa suluhu la vitendo badala ya adhabu.
Kwa nini Hakimu wa Thika alikataa kumtia hatiani mwanafunzi? Alipouliza kuhusu thamani ya whisky, mwendesha mashtaka alijibu kuwa ni KSh1,000 kabla ya kusahihisha na kugundua kuwa KSh1,800 zilionekana kwenye karatasi ya mashtaka.
Alimkumbusha kijana huyo kwamba kosa dogo mara nyingi hukua na kuwa mzigo wa muda mrefu mara moja linaporekodiwa kama hatia.
Baada ya kuuliza na kuthibitisha umri wake, Atambo alimwambia bado ana maisha marefu na aepuke makosa ambayo yamesalia kwenye faili rasmi. "Wameandika KSh1,800. Unajua ikifika kwa charge sheet inakuwa more expensive. Si uwalipe tu, tuachane na story nyingi, ju hii itakuwa record of previous conviction. Uko na miaka mingapi? Miaka 23, bado wewe ni mchanga sana," alisema.
Mwanafunzi huyo aliiambia mahakama kuwa alipendelea kulipa pesa hizo badala ya kufungwa jela, lakini alikosa pesa kwa vile hakuwa na kazi. Alipouliza ikiwa kuna mtu yeyote alikuja kumsaidia kulipa dhamana ya pesa taslimu, alisema binamu yake alikuwa akielekea kortini.
Kisha akabadilisha mjadala, akieleza kwamba alitaka kumtia hatiani kwa kutumia chupa ya whisky ya John Barr. "Je, hutaki ulipe pesa za duka kuu sasa. Nikuwachilie. Wamesema KSh 1,800; whisky inaitwa nini? Unajua hii inaitwa John Barr Whisky. Sitaki ujibu maombi yako na kukuhukumu kwa sababu ya chupa ya whisky," Atambo aliambia mahakama.
Jinsi gani Hakimu wa Thika alimwokoa mwanafunzi kutoka katika hatia Akiwageukia mawakili waliokuwepo kortini, Atambo alihoji wangeweza kumfanyia nini kwani alikuwa kijana anayehitaji mwelekeo.
Mawakili hao walisema walikubaliana na hakimu, wakieleza kuwa kiasi hicho kilitakiwa kumalizwa na duka kubwa.
Hakimu Atambo aliwakazia zaidi na kuwakumbusha madai yao ya mara kwa mara kuhusu kuwashauri vijana. "Wakili unamfahamu huyo? Humjui.
Lakini huyu hapa mtoto wa kiume mwenzako. Unaweza kumfanyia nini?" aliuliza. Hakimu huyo alionekana kuhalalisha kitendo cha mwanafunzi huyo, na kuongeza kuwa kuna uwezekano alitaka muda mfupi wa kupumzika na akaishia kufanya uamuzi mbaya.
Kundi la mawakili lilikubali kukusanya pesa ili kupata KSh1,800 huku wakisubiri binamu kuwasili.
Wakili mmoja alisema maafisa wangemrejesha kwenye seli huku wakishauriana jinsi ya kulipa kiasi hicho.
Hakimu Atambo alitumia muda huo kumtia moyo kujifunza kutokana na usaidizi ulioonyeshwa na wataalamu wakubwa katika chumba hicho.
Alimweleza mwanafunzi kwamba hatia ingechafua rekodi zake na kupunguza fursa za siku zijazo. "Unaona sasa hawa ni kaka zako wakubwa. Wanajua maana yake unapoiba whisky tu ili upate wakati mzuri na kupumzika. Wakufanyie kitu maana nikikutia hatiani itachafua rekodi yako. Ona ni sawa," aliongeza.
Alimwagiza awasiiane na binamu yake na akamhakikishia kwamba mawakili walikuwa tayari kumsaidia kulipa kiasi hicho. Mpangilio huo ulimaanisha kuwa mwanafunzi angefidia duka kuu bila kupokea rekodi ya uhalifu.
MABASI YA ESTER SIO YANGU WALA MKE WANGU: MWIGULU

Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, amevunja ukimya kuhusu uvumi unaoenezwa na baadhi ya watu kwamba mabasi ya kampuni ya Ester ni mali yake akisema jambo hilo sio la kweli na kuwataka Watanzania kutokubali kila wanachoelezwa.
“Siku hizi watu hawaogopi hata kusingizia jambo unakuta mtu hafanyi hata utafiti juu ya mtu anayetaka kumsema, juzi juzi nikasikia tumechoma magari ya Ester ya mbunge wa Iramba Magharibi, magari yake yanaitwa Ester ameyaita Ester jina la mke wake,”…
“Mke wangu mimi haitwi Ester anaitwa Neema, wanasema basi kama sio ya mke wake yatakuwa ya mama yake mama yangu binti wa kiislamu anaitwa Asha Ramadhani Mohamed,”
Dk.Mwigulu ambaye ametoa ufafanuzi huo IJUMAA ya Novemba 21, 2025 wakati akizungumza na mamia ya wananchi kwenye viwanja vya Bombadia Manispaa ya Singida, amesema yeye amezaliwa katika familia ya kifugaji ambayo huruhusiwi hata kufanya biashara ya miwa hivyo hajawahi kufanya biashara yeyote.
“Nimeingia huku serikalini uwekezaji mkubwa ninaoufanya ni kusomesha watoto na nina kundi la watoto zaidi ya 500 ninaowasomesha, nimewekeza kwenye huduma za watu,”amesema Dk.Mwigulu.
MBUNGE JIMBO LA KIBAHA VIJIJINI ATUA KWA KISHINDO NA KUTEMA CHECHE KWA WANANCHI
NA VICTOR MASANGU, KIBAHA
Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijiji Homoud Jumaa ameahidi kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) kwa vitendo ikiwemo kusimamia suala zima la kuwahudumia wananchi ipasavyo katika mambo mbali mbali kwa ajili ya kuwaletea chacu ya maendeleo katiika nyanja tofauti.
Jumaa ameyabainisha hayo wakati wa halfa fupi ya kumpokea rasmi kutokea Mkoani Dodoma ikiwa ni siku chache zimepita baada ya kuapishwa rasmi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini ambapo sherehe hiyo imehudhuliwa na na viongozi wa chama cha mapinduzi, wananchama pamoja na wananchi kutoka maeneo tofauti.
Mbunge huyo amesema kwamba kwa sasa uchaguzi umeshamalizika na kwamba kitu kikubwa amewaomba wanachama wote na wananchi kuhakikisha kwamba wadumisha hali ya amani na utulivu wa nchi na kuepukana na vurugu ambazo hazina maana na badala yake washikamane katika kukijenga chama pamoja na kushiriki kikamilifu katika mambo ya kimaendeleo.
"Nawashukuru kwa dhati viongozi wangu wa chama cha mapinduzi, wanachama wa ccm pamoja na wananchi wote kwa kuweza kuniamini kwa mara nyingine na kuweza kunipitisha tena kuwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kitu kikubwa ambacho ninaweza kuwaahidi ni kuendelea kutoa ushirikianio wa hali na mali katika kuhakikisha ninawaletea maendeleo mbali mbali,"amesema Jumaa.
Katika hatua nyiingine Mbunge huyo amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. kwa kuweza kuchaguliwa kwa kishindo pamoja na kuweza kutoa hotuba yake nzuri ambayo imelenga kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi katika sekta mbali mbali.
Kwa upande wake Diwani mteule wa kata ya Kwala Mansuri Kisebengo amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini kwa kuweza kuchaguliwa kwa kishindo na wananchi na kwamba ana imani kubwa wataweza kuwatumikia wananchi na kuwaletea chachu ya maendeleo.
Nao baadhi ya wananchi ambao wamepata fursa ya kuhudhulia katika halfa hiyo wamesema kwamba wana imani kubwa na serikali mpya ya awamu ya sita pamoja na kumpongeza Mbunge wa Jimbo hilo la Kibaha vijijini Hamoud Jumaa kwani ataweza kuleta mafanikio ya kimaendeleo kwa wananchi wake.
Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijni Mhe. Hamoud Juma amepokelewa kwa kishindo kikubwa na viongozi CCM, wananchama pamoja na wananchi sambamba na madiwani mbali mbali za Jimbo la KIbaha vijijini.
Monday, October 27, 2025
SERIKALI MKOA WA PWANI YAJIIMARISHA KWA ULINZI NA USALAMA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
VICTOR MASANGU, PWANI ... HABARI ..OCTOBA 27 /2025
SERIKALI Mkoa wa Pwani imesema kwamba imejiandaa vya kutosha hususan katika hali ya ulinzi na usalama katika kuelekea katika uchagzuo mkuu wa mwaka 2025 ambaop unatarajiwa kufanyika octoba 29 mwaka huu ambayo itakuwa ni siku ya jumatano ya wiki hii.
Hayo yamebaishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge wakati akizunhgumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na maandalizi ya kuelekea katika uchagzuzi huo ambapo amewaahimiza wanananchi wote wenye sifa kujitokeza kwa wingi kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.
Saturday, October 25, 2025
WANANCHI MWANZA WAHIMIZA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Makundi mbalimbali ya wananchi jijini Mwanza yamejitokeza kwa wingi na kushiriki kongamano la kuhamasisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
Kongamano hilo limeandaliwa na makundi hayo ambayo ni pamoja na machinga, bodaboda, wamiliki wa daladala, mama lishe na watu wenye ulemavu chini ya mlezi wao, Stanslaus Mabula ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana kwa awamu mbili kuanzia mwaka 2015/ 20225.
"Niwaombe kila mmoja tuendelee kudumisha amani ya nchi yetu, bila amani hata pikipiki zetu hatuwezi kuziendesha, amani yetu ndiyo maisha yetu" amesema Mwenyekiti wa waendesha bodaboda Mkoa wa Mwanza, Mohamed Idd akihimiza wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani.
Naye Katibu wa Machinga Mkoa wa Mwanza, Zuena Mahamudu amewahimiza wananchi kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani wakati wa uchaguzi na badala yake wakashiriki zoezi la kupiga kura kwa wingi kwa mstakabali wa maisha yao.
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)












